Wednesday, August 22, 2012

Je Kumpiga Mwenzi wako Ni suluhu ya matatizo yenu?



Na Frank Joachim

Katika Asilimia 100 ya Jinsia ambayo huwa wanapigwa sana katika Ndoa, Uchumba, Mapenzi ya Kawaida (Girlfriends and Boyfriends), Wanawake huwa wanachukua zaidi ya Asilimia 90. Kiafrika, hii huwa inatokana na Asilia tuliyokua nayo, yaani mfumo Dume.
Ni sawa, hata Ughaibuni mambo haya hutokea, japo ni kwa asilimia ndogo, kutokana na Sheria nza Nchi Hizo, Mfano Marekani, ukimpiga Mwanamke, basi unafunguliwa mashitaka ya “Domestic Violence” na Kuwajibishwa vilivyo. Hii inakuwa inawafanya watu wengi kuepukana na mtukio hayo ya uonevu wa Kijinsia.

Kwa Nini Tunapiga (Wanaume)



Kulinda Hadhi na Heshima.
Hakuna Jinsia ambayo huwa inathamini hadhi yake binafsi kama Jinsia Ya Kiume. Hii inatokana na mfumo dume uliorithishwa na Wazazi wetu wa Awali, yaani Mababu zetu, ambapo huwa mwanaume anahisi kuwa yeye ni bora na anastahili kuboreshewa ubora wake ili kutambulika katika Jamii inayomzunguka.
Endapo Mwanamke ataonesha dharau, Kiburi, kutokutekeleza baadhi ya Majukumu aliyokabidhiwa na Mwanamume (Mpenzi, mchumba, au Mume), basi ataadhibiwa kwa Kipigo chochote kile ili kuilinda Hadhi yake na Heshima yake isije ikashuka.

Hasira za Karibu

Hii ni sawa kabisa, hasa kwa Wanaume. Kuna baadhi ya Wanaume ambao kiujumla huwa ni Wepesi wa kuchukia haraka, na kuchukua hatua kadhaa mkononi. Kuna baadhi ya Wanaume ambao huwa hawafanyi hivyo. Mwanaume wa aina hii (Kuchukia Mapema) mara nyingi huwaadhibu sana Wapenzi wao. Nimewahi kuishi na rafiki yangu wa aina hii. Ilikuwa ikipita wiki Nzima mpenzi wake hajalia, basi jamaa atakuwa hayupo, au anaumwa. Jambo hili lilikuwa likimnyima raha sana Mpenzi wake, kitu ambacho kingepa athari kubwa ya Kisaikolojia Msichana Yule, endapo wasingetengana

Ulimbukeni/ Kuiga/ Sifa za Kijinga.

Kuna mwanaume mwingine anaweza akawa anahisi ni sifa mbele ya wenzake kusema kuwa amempiga mpenzi wake. Hii ni kutaka kujionesha kuwa ana mamlaka makubwa sana na ni sifa madhubuti kumpiga Mwenzi wake. Mwingine anaweza akawa anamuona Frank anapiga sana Mpenzi wake, na bado wanaendelea kuwa pamoja, basi na yeye anaamua kumpiga Ngum,I, makofi n.k ilimradi tu awe kama Frank, jambo ambalo sio unjanja wala nini !!

 Kwa nini anapenda Kupigwa? (Wanawake)

Kudhirisha kama anapendwa.

Zamani nilikuwa Siamini kama mwanamke anapenda kupigwa. Nilikuwa ninadhani kuwa wanawasikinzia. Katika Mapenzi ya sasa Hivi, yaani Rika letu sisi vijana, Nilibaini kuwa, kuna wanawake au mabinti wanapenda na huwa wanalazimisha kupigwa kwa kufanya makosa maksudi. Hii ni kutaka kubaini kama mpenzi wake anampenda au Laa.

Kuiga/ Ulimbukeni

Amini Usiamini, kuna wanawake ambao wakisika wenzao wakisimulia kuwa wamepigwa basi wanafurahi na kutramani na wao kupigwa. Basi watafanya kila wafanyalo au wawezalo ili kuhakikisha kuwa wanapigwa na wapenzi wao ili kujua radha yake ikoje.

ATHARI;

Athari huwa ni kubwa sana katika Hilo.
Kujeruhi
Kuua,
Kuathiri/ Kuathirika Kisaikolojia., n.k

No comments:

Post a Comment